Meal Seç / Sure Seç

AZ-ZILZALAH Suresi

(SWAHILI) QURAN


99 - AZ-ZILZALAH
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
        
1. Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
3. Na mtu akasema: Ina nini?
4. Siku hiyo itahadithia khabari zake.
5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
6. Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
KURAN uygulamasını telefonunuza siz de yükleyin: