(SWAHILI) QURAN |
| 96 - AL - A'LAQ |
| KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
|
| 1. | Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, |
| 2. | Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, |
| 3. | Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! |
| 4. | Ambaye amefundisha kwa kalamu. |
| 5. | Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui. |
| 6. | Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri |
| 7. | Akijiona katajirika. |
| 8. | Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo. |
| 9. | Umemwona yule anaye mkataza |
| 10. | Mja anapo sali? |
| 11. | Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu? |
| 12. | Au anaamrisha uchamngu? |
| 13. | Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma? |
| 14. | Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona? |
| 15. | Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele! |
| 16. | Shungi la uwongo, lenye makosa! |
| 17. | Basi na awaite wenzake! |
| 18. | Nasi tutawaita Mazabania! |
| 19. | Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee! |