(SWAHILI) QURAN |
| 90 - AL - BALAD |
| KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
|
| 1. | Naapa kwa Mji huu! |
| 2. | Nawe unaukaa Mji huu. |
| 3. | Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa. |
| 4. | Hakika tumemuumba mtu katika taabu. |
| 5. | Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza? |
| 6. | Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali. |
| 7. | Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona? |
| 8. | Kwani hatukumpa macho mawili? |
| 9. | Na ulimi, na midomo miwili? |
| 10. | Na tukambainishia zote njia mbili? |
| 11. | Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. |
| 12. | Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? |
| 13. | Kumkomboa mtumwa; |
| 14. | Au kumlisha siku ya njaa |
| 15. | Yatima aliye jamaa, |
| 16. | Au masikini aliye vumbini. |
| 17. | Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana. |
| 18. | Hao ndio watu wa kheri wa kuliani. |
| 19. | Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni. |
| 20. | Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande. |