(SWAHILI) QURAN SURE SEÇİNİZ
![]() ![]() (SWAHILI) QURAN |
104 - AL - HUMAZAH |
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
![]() ![]() ![]() ![]() |
1. | Ole wake kila safihi, msengenyaji! |
2. | Aliye kusanya mali na kuyahisabu. |
3. | Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! |
4. | Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. |
5. | Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? |
6. | Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. |
7. | Ambao unapanda nyoyoni. |
8. | Hakika huo utafungiwa nao |
9. | Kwenye nguzo zilio nyooshwa. |