(SWAHILI) QURAN SURE SEÇİNİZ
(SWAHILI) QURAN |
| 101 - AL - QAARIA'H |
| KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
|
| 1. | Inayo gonga! |
| 2. | Nini Inayo gonga? |
| 3. | Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? |
| 4. | Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; |
| 5. | Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! |
| 6. | Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, |
| 7. | Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. |
| 8. | Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, |
| 9. | Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! |
| 10. | Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? |
| 11. | Ni Moto mkali! |