1. |
Litakapo tukia hilo Tukio
|
2. |
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
|
3. |
Literemshalo linyanyualo,
|
4. |
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
|
5. |
Na milima itapo sagwasagwa,
|
6. |
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
|
7. |
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
|
8. |
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
|
9. |
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
|
10. |
Na wa mbele watakuwa mbele.
|
11. |
Hao ndio watakao karibishwa
|
12. |
Katika Bustani zenye neema.
|
13. |
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
|
14. |
Na wachache katika wa mwisho.
|
15. |
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
|
16. |
Wakiviegemea wakielekeana.
|
17. |
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
|
18. |
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
|
19. |
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
|
20. |
Na matunda wayapendayo,
|
21. |
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
|
22. |
Na Mahurulaini,
|
23. |
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
|
24. |
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
|
25. |
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
|
26. |
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
|
27. |
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
|
28. |
Katika mikunazi isiyo na miba,
|
29. |
Na migomba iliyo pangiliwa,
|
30. |
Na kivuli kilicho tanda,
|
31. |
Na maji yanayo miminika,
|
32. |
Na matunda mengi,
|
33. |
Hayatindikii wala hayakatazwi,
|
34. |
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
|
35. |
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
|
36. |
Na tutawafanya vijana,
|
37. |
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
|
38. |
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
|
39. |
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
|
40. |
Na fungu kubwa katika wa mwisho. 3
|
41. |
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
|
42. |
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
|
43. |
Na kivuli cha moshi mweusi,
|
44. |
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
|
45. |
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
|
46. |
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
|
47. |
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
|
48. |
Au baba zetu wa zamani?
|
49. |
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
|
50. |
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
|
51. |
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
|
52. |
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
|
53. |
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
|
54. |
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
|
55. |
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
|
56. |
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
|
57. |
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
|
58. |
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
|
59. |
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
|
60. |
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
|
61. |
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
|
62. |
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
|
63. |
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
|
64. |
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
|
65. |
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
|
66. |
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
|
67. |
Bali sisi tumenyimwa.
|
68. |
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
|
69. |
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
|
70. |
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
|
71. |
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
|
72. |
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
|
73. |
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
|
74. |
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
|
75. |
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
|
76. |
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
|
77. |
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
|
78. |
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
|
79. |
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
|
80. |
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
81. |
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
|
82. |
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
|
83. |
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
|
84. |
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
|
85. |
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
|
86. |
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
|
87. |
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
|
88. |
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
|
89. |
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
|
90. |
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
|
91. |
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
|
92. |
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
|
93. |
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
|
94. |
Na kutiwa Motoni.
|
95. |
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
|
96. |
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
|