1. |
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
|
2. |
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
|
3. |
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
|
4. |
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
|
5. |
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
|
6. |
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
|
7. |
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
|
8. |
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
|
9. |
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
|
10. |
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
|
11. |
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
|
12. |
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
|
13. |
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
|
14. |
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
|
15. |
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
|
16. |
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
|
17. |
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
|
18. |
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
|
19. |
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
|
20. |
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
|
21. |
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
|
22. |
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
|
23. |
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
|
24. |
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
|
25. |
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
|
26. |
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
|
27. |
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
|
28. |
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
|
29. |
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
|
30. |
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
|
31. |
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
|
32. |
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
|
33. |
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
|
34. |
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
|
35. |
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
|
36. |
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
|
37. |
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
|
38. |
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
|
39. |
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
|
40. |
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
|
41. |
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
|
42. |
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
|
43. |
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
|
44. |
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
|
45. |
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
|
46. |
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
|
47. |
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
|
48. |
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
|
49. |
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
|
50. |
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
|
51. |
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
|
52. |
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
|
53. |
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
|
54. |
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
|
55. |
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
|