Meal Seç / Sure Seç

ASH-SHAMS Suresi

(SWAHILI) QURAN


91 - ASH-SHAMS
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
        
1. Naapa kwa jua na mwangaza wake!
2. Na kwa mwezi unapo lifuatia!
3. Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
4. Na kwa usiku unapo lifunika!
5. Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
6. Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
7. Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
8. Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
9. Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
10. Na hakika amekhasiri aliye iviza.
11. Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
12. Alipo simama mwovu wao mkubwa,
13. Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
14. Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
15. Wala Yeye haogopi matokeo yake.
KURAN uygulamasını telefonunuza siz de yükleyin: