(SWAHILI) QURAN |
| 86 - ATT'AARIQ |
| KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
|
| 1. | Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku! |
| 2. | Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku? |
| 3. | Ni Nyota yenye mwanga mkali. |
| 4. | Hapana nafsi ila inayo mwangalizi. |
| 5. | Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani? |
| 6. | Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa, |
| 7. | Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu. |
| 8. | Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha. |
| 9. | Siku zitakapo dhihirishwa siri. |
| 10. | Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi. |
| 11. | Naapa kwa mbingu yenye marejeo! |
| 12. | Na kwa ardhi inayo pasuka! |
| 13. | Hakika hii ni kauli ya kupambanua. |
| 14. | Wala si mzaha. |
| 15. | Hakika wao wanapanga mpango. |
| 16. | Na Mimi napanga mpango. |
| 17. | Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole. |