1. |
Naapa kwa mlima wa T'ur,
|
2. |
Na Kitabu kilicho andikwa
|
3. |
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
|
4. |
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
|
5. |
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
|
6. |
Na kwa bahari iliyo jazwa,
|
7. |
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
|
8. |
Hapana wa kuizuia.
|
9. |
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
|
10. |
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
|
11. |
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
|
12. |
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
|
13. |
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
|
14. |
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
|
15. |
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
|
16. |
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
|
17. |
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
|
18. |
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
|
19. |
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
|
20. |
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
|
21. |
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
|
22. |
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
|
23. |
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
|
24. |
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
|
25. |
Wataelekeana wakiulizana.
|
26. |
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
|
27. |
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
|
28. |
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
|
29. |
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
|
30. |
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
|
31. |
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
|
32. |
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
|
33. |
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
|
34. |
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
|
35. |
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
|
36. |
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
|
37. |
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
|
38. |
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
|
39. |
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
|
40. |
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
|
41. |
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
|
42. |
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
|
43. |
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
|
44. |
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
|
45. |
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
|
46. |
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
|
47. |
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
|
48. |
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
|
49. |
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
|