(SWAHILI) QURAN SURE SEÇİNİZ
![]() ![]() (SWAHILI) QURAN |
93 - WADH-DHUH'AA |
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
![]() ![]() ![]() ![]() |
1. | Naapa kwa mchana! |
2. | Na kwa usiku unapo tanda! |
3. | Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe. |
4. | Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia. |
5. | Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike. |
6. | Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi? |
7. | Na akakukuta umepotea akakuongoa? |
8. | Akakukuta mhitaji akakutosheleza? |
9. | Basi yatima usimwonee! |
10. | Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! |
11. | Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie. |