(SWAHILI) QURAN SURE SEÇİNİZ
(SWAHILI) QURAN |
| 99 - AZ-ZILZALAH |
| KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
|
| 1. | Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake! |
| 2. | Na itakapo toa ardhi mizigo yake! |
| 3. | Na mtu akasema: Ina nini? |
| 4. | Siku hiyo itahadithia khabari zake. |
| 5. | Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia! |
| 6. | Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao! |
| 7. | Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! |
| 8. | Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! |